Zifuatazo ni kanuni 10 za ndoa bora.
1. KANUNI YA NENO LA KUPENDEZA
Usipitishe siku nzima bila kutamka neno la kupendeza na la kukumbukwa na mwenzio kwa muda wote ambao hautakuwepo. Soma Mithali 17:22 na Mithali 10:1
2. KANUNI YA NENO “NIMEFURAHI KUKUONA”
Usikutane na mwenzio bila kumkaribisha kwa kauli ya upendo. Soma Mwanzo 18:2-3 na Mwanzo 19:16-20
3. KANUNI YA KUTAWALA HASIRA
Usiwe mwepesi wa kukasirika. Soma Mithali 14: 17-18, Mithali 16:32, Yakobo 1:19.
4. KANUNI YA KUDHIBITI ULIMI.
Usiongee kwa sauti kubwa na mwenzako. Soma, Mithali 10:32, Mithali 17:28 na Mithali 19:29
5. KANUNI YA UWAJIBIKAJI
Usiruhusu mwenzio arudie kuuliza swali. Soma, Mithali 12:4, 26.
6. KANUNI YA UKARIMU
Usifanye Jambo kwa gharama za wengine. Mithali 3: 27-28.
7. KANUNI YA UTII
Wapenzi wawili mko sawa. Ni mameneja wawili ambao kila mmoja ana majukumu yake ndani ya taasisi moja iitwayo ndoa. Soma, Mwanzo 3:16-19.
8. KANUNI YA KUZIKA MAKOSA
Usifufue makosa, labda kama yanajirudia mara kwa mara. Siku zote ongea kwa upendo kuhusu hilo. Mithali 21:16
9. KANUNI YA USAFI WA JAMBO
Siri ya furaha iko kwenye kusahau yaliyopita na kuanza kila siku na mambo safi. Soma, Mithali 17:1
10 KANUNI YA MUUNGANO WA THAMANI
Muda wote ukiwa na nafasi kaa na mwenzi wako. Soma Mwanzo 2:24.
INALIPA