Maandiko yanatuambia katika Biblia Takatifu
Mith 23:7a “Aonavyo nafsini mwake ndivyo alivyo”.
Je wewe unaona nini mbele yako? Siku zote huwezi kuona kwenye moyo wako tofauti na kile unachokula kwa kusikia, kutazama ama kuhisi
Hii ndio sababu ninashauri watu wajifunze kuwa na vitu positive wanavyojishugulisha navyo kila siku kwenye maisha yao, maana kama wewe unasikia mambo ya mauti, unaona mambo ya mauti, unahisi mambo ya mauti ni rahisi kuota hata umekufa au uko kwenye jeneza ukasema nguvu za giza kumbe nafsi yako imejaa ayo mambo .
Marafiki wanaokuzunguka wanajaza nini kwenye nafsi yako, maana wanachokijaza kitakuwa na mchango mkubwa katika mtazamo wako kimaisha , mazingira yanayokuzunguka yanajaza nini katika nafsi yako, filamu unazo anagalia zinajaza nini, nyimbo unazo sikiliza mara kwa mara zinajaza nini katika nafsi yako, maana kama unakaa na watu waliokata tamaa uwe na uhakika hata maisha yako yatakuwa ni ya kukata tamaa tu.
Kama wewe ni mwana ndoa na mda mwingi unautumia kukaa na walioachika unaweza ukajikuta umeanza kubadilika kimtazamo, Ndio sababu Biblia ikasema katika;
1 Timoth 4:16 “Jitunze nafsi yako na mafundisho yako…”
Unajitunzaje ni kwa kuwa makini na vitu utakavyokuwa ukiviruhusu kuingia katika nafsi yako, kumbuka kuona kwako, kesho yako itategemea nini unakipa nafasi katika nafsi yako leo.